» » Jiulize, Kama ungekufa leo, Ungeenda wapi?


Jiulize, Kama ungekufa leo, Ungeenda wapi?
Uamuzi Sahihi Utakaoufurahia Milele
www.zakachekainjili.blogspot.com

KWANINI?
Utakapokufa, hautapotea tu. Utaingia katika maisha mengine ya umilele mahali Fulani. Mbingu ipo na Motoni kupo pia. Watu hawapendi kuzungumzia kuhusu motoni au kufikiri  kuhusu huko. Lakini ni kweli kabisa Jehanum ipo. Na tunapaswa kuizungumzia ili kila mmoja ajue na aweze kufanya maamuzi sahihi.

Mbinguni ni mahali kwa wale waliosamehewa makosa yao na Mungu. Na motoni ni kwa wale ambao hawajapata msamaha huo.
Mungu ni mwema, Mungu Baba anataka uwe na uhusiano mzuri nay eye na hatimaye uurithi uzima wa milele Mbinguni ambako kila kitu ni chema.

Unawezaje kupata msamaha kutoka kwa Mungu?

YESU
Njia pekee ya kupata msamaha wa dhambi zako ni Yesu. Yesu ni mwana wa Mungu. Aliyatoa maisha yake na kuwa tayari kufa msalabani kwa ajili ya dhambi  zetu wanadamu. Yesu aliipa deni la maovu yetu  na kwa jinsi hiyo tunapata msamaha wa maovu yetu kwa Mungu.

Lakini msamaha hauji tu wenyewe. Unapaswa umkiri Yesu kuwa Mwokozi wa Maisha yako ndipo upate msamaha.


Unawezaje kumkiri Yesu kuwa Mwokozi wako?


SASA
Unaweza Kumkiri Yesu kuwa Mwokozi wa Maisha yako sasa hivi kwa kuomba sala ifuatayo. Tamka kwa sauti, sema maneno yote kwa moyo wako wote.

Sala ya Msamaha wa Dhambi
“Mungu, nisamehe kwa makosa niliyoyatenda. Nakuomba unisamehe. Yesu, Wewe ni Mwana wa Mungu. Ahsante kwa kulipa deni la dhambi zangu kwa kifo chako msalabani. Naamini ulifufuka kutoka mautini na sasa uko Mbinguni. Nakukubali uwe Bwana na Mwokozi wa Maaaisha yangu. Yesu, Nakualika ukae name maishani mwangu sasa katika jina la Yesu Amen!”

Kama umeomba sala hii kwa kumaanisha, umesamehewa na uhusiano wako na Mungu umerejea upya tena. Na kupitia uhusiano huu sahihi na Mungu utaenda Mbinguni na Kuishi Maisha ya Umilele huko. Hongera! Hakikisha unabonyeza maneno meusi hapa chini yaliyoandika HATUA YA 2 kwa msaada zaidi wa kiroho ili uzidi kukua na kumjua Yesu zaidi.

Kama umemkubali Yesu kuwa Mwokozi wako baada ya kusoma ujumbe huu, tunapenda kusikia kutoka kwako! Pia kila mmoja anakaribishwa kuchangia maoni yake pamoja nasi. Unaweza kutufikia kwa kutumia email ifuatayo: zacharybequeker@gmail.com 


Pakua App Ya Injili Halisi -Bofya Hapa Flower
HII NI INJILI HALISI MINISTRY, KWA MAWASILIANO +255 621 261 295

About INJILI HALISI MINISTRY

Zachary, most known as Zakacheka is the founder of the Injili Halisi Ministry. He is a member of Full Gospel Bible Fellowship Church.. He lives in Mwanza,Tanzania. 0621261295.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply