» » MADHARA YA KUVUNJA AHADI NA KUTOKUONDOA NADHIRI

Na Kaka Zachary +255625966236
Katika somo hili tutajifunza mambo yafuatayo:
  Ø  Nini Maana ya ahadi na nadhiri?
  Ø  Mifano wa walioahidi na kuweka nadhiri katika biblia
  Ø  Madhara yatokanayo na kuvunja ahadi na kutoondoa nadhiri

NINI MAANA YA AHADI NA NADHIRI

AHADI ni sharti alilojipa mtu kulitimiza; agano, mapatano. Ahadi inapotamkwa ni lazima itimizwe.

NADHIRI ni ahadi au kauli rasmi kabisa ya kufanya ya kutofanya jambo fulani kwa Mungu.
Mungu huwaadhibu wale washindwao kutimiza ahadi hiyo(nadhiri)

MIFANO WA WATU WALIOAHIDI NA KUWEKA NADHIRI ZAO MBELE ZA MUNGU
Katika biblia kuna watu wengi walioweka nadhiri zao mbele za Bwana. Hapa tutawaangalia baadhi yao tu:

Wa kwanza ni Hana alikuwa ni mke wa Elkana na alipendwa sana na mmewe lakini kwa sababu hakuwa na mtoto, mke mwenzio Penina alikuwa akimnyanyasa sana. Kitendo hiki kilimfadhaisha sana Hana akawa ni mtu mwenye huzuni wakati wote, alilia sana. Hatimaye akaona kulia tu haisaidii kitu ndipo akaona amwendee Muumba wa vyote, aliye mwisho wa fedheha, Bwana wa mabwana. Kwa jinsi alivyokuwa akiomba alionekana kana kwamba amelewa kumbe la bali ni kwa sababu alivyokuwa amezama katika maombi. Alimuomba Mungu na akaweka nadhiri kwamba akipewa mtoto atamtoa mtoto huyo awe ni wa Bwana miaka yote na ndivyo alivyofanya “Naliomba nipewe mtoto huyu; Bwana akanipa dua yangu niliyomwomba;kwa sababu hiyo mimi nami nimempa Bwana mtoto huyu; wakati wote atakaokuwa hai amepewa Bwana. Naye akamwabudu Bwana huko.” (1 SAMWELI 1:9-28)

Wa pili ni Yeftha alikuwa akienda kupigana vitani ndipo akamwekea Bwana nadhiri, akasema, “Kwamba wewe utawatia wana wa Amoni mkononi mwangu kweli,ndipo itakuwa ya kwamba, kile kitakachotoka katika milango ya nyumba yangu kunilaki, hapo nitakaporudi na amani kutoka kwa hao wana wa Amoni, kitu hicho kitakuwa ni cha Bwana, nami nitakisongeza kiwe sadaka ya kuteketezwa”. Bwana alimsaidia akawapiga adui zake wote, pindi anarudi aliyetoka wa kwanza kumlaki alikuwa ni binti yake na mtoto wake wa pekee, na kumbuka katika ahadi yake alisema kitakachotoka katika malango ya nyumba yake kumlaki atakaporudi salama atakitoa sadaka ya kuteketezwa;. Yeftha alisononeka sana moyoni lakini kwa sababu alijua madhara ya kutotimiza ahadi ili mlazimu amtoe mwanae wa pekee sadaka na hivyo akabaki bila mtoto. (WAAMUZI 11:30-40)

Wa tatu ni Yakobo aliweka nadhiri kwa Mungu wakati wa safari yake akielekea Padan-aramu, katika nyumba ya babu yake Bethueli (baba yake na mama yeke) akajitwalie huko mke katika binti za Labani, ambaye alikuwa ni kaka yake na mama yake yaani mjomba wake. Isaka baba yake, hakupenedelea kumuona Yakobo akioa wanawake wa Kikanaani ndipo akamuagiza huko(MWANZO 28:20-22).

MADHARA YA KUVUNJA AHADI NA KUTOTIMIZA NADHIRI

Kuvunja ahadi ni dhambi kama ilivyo dhambi ya uongo (HOSEA 4:2-3), Kwa sababu unapovunja ahadi unadhihirisha kwamba kile ulichokisema kilikuwa si cha kweli bali ni uongo na biblia inakataza kusema uongo(WAKOLOSAI 3:9). Kuna watu wanatabia yakuwaahidi watu kuwatendea jambo fulani na wala hawatendi, hiyo ni dhambi kama dhambi zingine na inatosha kabisa kukupeleka motoni. Kama ulimahidi mtu na hukutimiza nakushauri utimize ahadi yako la sivyo laana inakukalia pamoja na kwamba vitu ni vya kwako lakini unakuwa mdaiwa kwa sababu wasawahili husema ahadi ni deni. Kumbe unapomuahidi mtu wala hutimizi unakuwa unadaiwa na biblia inatuambia akopaye ni mtumwa wa Yeye amkopeshaye (MITHALI 22:7), ooooh kumbe wewe ni mtumwa tayari. Hebu kataa utumwa huo, fahamu wewe ni mtumwa wa Kristo pekee na si mtumwa wa mwanadamu, timiza ahadi. Kama Mungu hutimiza ahadi zake kwetu kwanini wewe usitimize? Je, wewe ni bora kuliko Mungu?

Unapoweka nadhiri mbele za Bwana kumbuka kuziondoa (ZABURI 76:11, ZABURI 116:14)
Kumbuka ulimwomba Mungu akupe kazi, mke, mme, watoto, nyumba, gari na ukaweka nadhiri kwamba akikupa utafanya hiki au hautafanya kile naye akakupa, ulimwomba akufanikishe katika mambo yako na sasa ametenda na umesahau kwamba ulimuahidia nini Bwana (AYUBU 22:27) Anayeiondoa nadhiri anabarikiwa na asiyeiondoa analaaniwa ubarikiwe (MAMBO YA WALAWI 22:21).

Madhara ya kutoondoa nadhiri zetu ni kifo
Anania na Safira waliahidi watauza kiwanja chao na kumtolea Bwana fedha yote ya mauzo ya kiwanja hicho. Baada ya kuuza hawakupeleka fedha yote na badala yake walificha na kupeleka kiasi fulani tu wakidhani Mungu hawaoni kumbe looo! Walijidanganya nafsi zao wenyewe. Mungu aliwaua wote wawili, mke na mme (MATENDO YA MITUME 5:1-11).  Unaweza kujisifu kwa ubingwa wako wa kuweka nadhiri na kuingia mitini wala hawakufuatilia, nakupa pole! Unaweza sema ‘mbona mimi sijafa’, kumbe Mungu ameshaua mambo mengine; inaweza kuwa ni kazi zako, biashara zako hazifanikiwi kwa sasa kumbe chanzo ni ile nadhiri, ndoa yako au masomo yako kuyumba kumbe chanzo ni ile nadhiri uliyoweka wala hukuiondoa. Mungu anaweza kukuua kimwili yaani afya, kikazi, kibiashara, kielimu au kwa namna yoyote ile. Kuna watu mmekuwa mkilalamika na kulalamika na kumlaumu Mungu bure kumbe tatizo ni ninyi wenyewe mnamfanyia Mungu uhuni eeee? Kumbuka Mungu hadhihakiwi. Mkumbuke Samsoni pamoja na kutembea na Mungu kwa miaka mingi lakini kosa moja tu lililomfanya kutiwa chini ya mikono ya Wafilisti haikuwa ni kulala na Delila bali ni kwa sababu alishindwa kuitunza nadhiri (WAAMUZI 13 na 16).

Kuna watu mnatabia ya kuwka nadhiri kanisani kwamba utatoa hiki au utafanya jambo fulani hali unaona uwezo wa kutimiza ahadi hiyo huna, unafanya ili watu wengine wakuone upigiwe na makofi mengi halafu mwishoni unaingia mitini, nawaambia dhambi hiyo ni mbaya bora hata kahaba neema ya Mungu inamvutavuta ili ampokee Kristo lakini kwako wewe si umemuona Mungu ni kauchunguro? Nakupa pole ndugu yangu. Nakushauri utubu na uziondoe nadhiri hizo ndipo utakuwa salama vinginevyo utazunguka mno kuombewa na kuombewa pasipo mafanikio.
Kama ni mtu anaomba umsaidie jambo fulani na unaona uwezo huna kuwa tu muwazi kuliko kumwambia ‘sawa nitakupa’ halafu usifanye hivyo. Nakuambia hapo hakuna namna, dawa ni kutoa tu.

MHUBIRI 5:4-5 “4 Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; kwa kuwa yeye hawi radhi na wapumbavu; basi, uiondoe hiyo uliyoiweka nadhiri.5 Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe.”


GROUP LA FACEBOOK: INJILI HALISI MINISTRY

Pakua App Ya Injili Halisi -Bofya Hapa Flower
HII NI INJILI HALISI MINISTRY, KWA MAWASILIANO +255 621 261 295

About INJILI HALISI MINISTRY

Zachary, most known as Zakacheka is the founder of the Injili Halisi Ministry. He is a member of Full Gospel Bible Fellowship Church.. He lives in Mwanza,Tanzania. 0621261295.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply