» » JINSI YA KUMPATA MUNGU MAISHANI MWAKO




Fahamu kwamba Mungu anakupenda!

Biblia inatuambia kwamba, Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” YOHANA 3:16

Tatizo ni kwamba…………

Wote tumetenda, tumewaza au kuzungumza maovu. Hii inaitwa dhambi, na dhambi zetu hututenganisha na Mungu wetu.

Biblia inasema katika WARUMI 3:23  “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.”  
Mungu ni mkamilifu na mtakatifu, na dhambi zetu hututenga sisi na Mungu milele. Biblia inasema “Mshahara wa dhambi ni mauti.”WARUMI 6:23

Habari njema ni kwamba, miaka 2,000 iliyopita,
Mungu alimtuma mwanae wa pekee Yesu Kristo ili afe kwa ajili ya dhambi zetu.

Yesu ni mwana wa Mungu. Aliishi maisha yasiyo ya dhambi hapa duniani kasha akafa msalabani ili kulipa deni za dhambi zetu.
“Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.”WARUMI 5:8

Yesu alifufuka kutoka katika mauti na sasa yu hai mbinguni pamoja na Mungu Baba. Alitupatia zawadi ya Uzima wa Milele – wa kuishi milele pamoja na Yeye mbinguni kama tukimkubali yeye kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yetu.

Yesu alisema “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.” – YOHANA 14:6

Mungu hudhihirisha pendo lake kwako na anakutaka wewe uwe mtoto Wake. “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.” – YOHANA 1:12. Unaweza kumuomba Yesu kristo akusamehe dhambi zako na awe katika maisha yako kama Bwana na Mwokozi.

Kama unataka kumpokea Kristo kama Bwana na Mwokozi na akuondoe katika dhambi zako, unaweza kumwomba kwa kufuatisha sala hii:

“Bwana Yesu, naamini wewe ni Mwana wa Mungu. Ahsante kwa kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu. Nakuomba unisamehe dhambi zangu zote na unipe zawadi ya uzima wa milele. Ninakuhitaji katika maisha yangu  na moyo wangu uwe Bwana na Mwokozi wangu. Nahitaji niyatenda matendo yako mema wakati wote katika jina lako Yesu Kristo Amen”


“Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe” – 1 YOHANA 5:11

Je, umefuatisha sala hii? Kama ni ndiyo bonyeza neno hili<<<NDIYO>>>  

© 2018 INJILI HALISI MINISTRY

Pakua App Ya Injili Halisi -Bofya Hapa Flower
HII NI INJILI HALISI MINISTRY, KWA MAWASILIANO +255 621 261 295

About INJILI HALISI MINISTRY

Zachary, most known as Zakacheka is the founder of the Injili Halisi Ministry. He is a member of Full Gospel Bible Fellowship Church.. He lives in Mwanza,Tanzania. 0621261295.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply