» » KWANINI DAUDI ALITUMIA MAWE MATANO KUMUUA GOLIATHI?

Goliathi na Daudi

I Samweli 17:31-40 inasema kwamba Daudi mwana wa Yese hakutaka kuvaa mavazi ya kivita na badala yake alichukua mawe matano ili kumuua Goliathi.

Kwanini Daudi alitumia mawe matano ili kumuua Goliathi?  Je, Daudi alimuogopa Goliathi? Jibu ni Hapana! Kumbuka Daudi alikuwa tayari alishaua dubu na simba kwa mikono yake mwenyewe. Kwa hiyo kama alikuwa anauwezo huo basi alikuwa ni mzoefu sana na mtu mwenye mbinu nyingi kwa habari ya kukabiliana na adui.

Daudi alikuwa akitokea katika ukoo wa Yuda. Alikuwa ameandaliwa vyema katika utumiaji wa kombeo wala hakuhitaji mawe mengi.
Waamuzi 20: 15-16 ‘’Hao wana wa Benyamini walihesabiwa siku ile kutoka hiyo miji, watu waume ishirini na sita elfu waliotumia upanga, zaidi ya hao waliokaa Gibea, ambao walihesabiwa watu wateule mia saba. Katika watu hao wote walikuwako watu waume mia saba waliochaguliwa, wenye shoto; kila mmoja alikuwa anaweza kuutupia unywele mawe kwa teo, wala asikose.’’

Unaposoma katika 2 Samweli 21:15-22 na  1 Mambo ya Nyakati 20:1-8 Tunaweza kukwambia kwamba Goliathi alikuwa na ndugu wanne, (Yeye alikuwa wa tano) Ishbi-Benobu, Safu, Lahmi, na jitu “Huge man”.  Wote hawa walikuwa ni majitu(giants) ambao walikuwa ni wana wa jitu lililoitwa  Mrefai  lililoishi Gathi.

Mrefai kwa biblia ya kiingereza inaandikwa Rapha ambayo kwa kiebrania inamaanisha GIANT yaani jitu kubwa, pandikizi (2 Samweli 21:22), Mrefai aliishi Gathi akiwa na vijana watano             (1 Nyakati 20:8): Goliathi (1 Samweli 17:23), Ishbi-Benobu(2 Samweli 21:16), Safu (1 Mambo ya Nyakati 20:4), Lahmi (1 Mambo ya Nyakati 20:5),  na  “jitu kubwa”,  Ambaye aliuliwa na askari wa Daudi huko  Gathi  (2 Samweli 21:20, 1 Mambo ya Nyakati 20:6).  Mtu huyu alikuwa ni hatari kwa sababu alikuwa ana vidole sita miguuni na mikononi.

Kulingana na kanuni na sheria za  Israeli, sheria ya vita ilitaka wapiganaji vita hodari wote kuingia katika vita na kulinda mipaka yao.  Hii inadhihirisha kwamba si Goliathi pekee aliyekuwa akiliwakilisha jeshi la Wafilisti katika bonde la Ela siku ya mapigano dhidi ya wapinzani wao bali pia na ndugu zake wane walikuwa pamoja naye. 

Goliathi hakuwa ametahiriwa. Goliathi alikuwa na ndugu wanne ambao hawakutahiriwa pia.
Inaonesha kwamba Daudi hakuwa pale ili kumuua  Goliathi pekee bali na ndugu zake wanne pia.

Hitimisho: " Naye Daudi akajifunga upanga juu ya mavazi yake, akajaribu kwenda; maana alikuwa hajavijaribu. Daudi akamwambia Sauli, Siwezi kwenda na vitu hivi, maana sikuvijaribu. Basi Daudi akavivua. Akaichukua fimbo yake mkononi, akajichagulia mawe laini matano katika kijito cha maji, akayatia katika mfuko wa kichungaji aliokuwa nao, maana ni mkoba wake, na kombeo lake alikuwa nalo mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti."    (1 Samweli 17:39-40).
Labda Daudi alichukua mawe matano kumuua Goliathi kwa sababu alikuwa na ndugu zake watano. Katika tamaduni za kale, kulikuwa na tabia iliyoitwa malipizo ya damu "blood revenge." Kama mtu alimjeruhi mtu fulani, baadaye ndugu wa mtu yule aliyejeruhiwa walikuja kufanya malipizo kwa adui. Hivyo Daudi alijua kama atamuua Goliathi na lazima ndugu zake wataingilia kati ili kulipiza kisasi, hivyo alijiandaa pia kupambana nao. 
" Kulikuwa na vita tena huko Gathi; ambako kulikuwa na mtu mrefu sana, mwenye vidole sita katika kila mkono, na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne; yeye naye alizaliwa kwa Mrefai. Naye huyo alipowatukana Israeli, ndipo Yonathani, mwana wa Shama, nduguye Daudi, akamwua. Hao wanne walizaliwa kwake huyo Mrefai wa Gathi; wakaanguka kwa mkono wa Daudi, na kwa mikono ya watumishi wake."   (2 Samweli 21:20-22).

------------------------------------------------------------------


Je, unataka kuokoka?
Tuma neno "NATAKA KUOKOKA" kwa SMS au WhatsApp kwa +255625966236
Facebook Group: Injili Halisi Ministry
KWA MAFUNDISHO TEMBELEA;
🔗zakachekainjili.blogspot.com
💕 Sharing is Caring💓

Pakua App Ya Injili Halisi -Bofya Hapa Flower
HII NI INJILI HALISI MINISTRY, KWA MAWASILIANO +255 621 261 295

About INJILI HALISI MINISTRY

Zachary, most known as Zakacheka is the founder of the Injili Halisi Ministry. He is a member of Full Gospel Bible Fellowship Church.. He lives in Mwanza,Tanzania. 0621261295.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply