» » OLE WAKE AKOSESHAYE


Ulimwenguni kuna mambo mengi yanayoweza kumkosesha mtu au kuwakosesha watu.
Pamoja na kwamba hayana budi kuja lakini ni ole kwake ayaletaye.
MATHAYO 18:7 7 Ole ni wa ulimwengu kwa sababu ya mambo ya kukosesha! Maana hayana budi kuja mambo ya kukosesha; lakini ole wake mtu yule aliletaye jambo la kukosesha!”

Mfano wa mambo yanayoweza kukosesha ni mafundisho potofu, mavazi, malezi mabaya,  mazungumzo mabaya na hata chakula pia. Hebu tuanze na moja baada ya jingine.
   1.      Mafundisho potofu humfanya mtu aamini uongo na kuufata na hatima yake huishia kupotea kwa sababu ni uongo. Biblia inatoa onyo juu ya wahubiri au walimu wafundishao upotofu kwa tamaa zao wenyewe.
   2.      Mavazi wanayovaa hasa wanawake wa leo ni mavazi yanayowavuta vijana kufanya uzinzi/uasherati. Wanawake inawapasa mvae mavazi yatakayowaokoa wanaume kuvutwa na tama kisha kutenda dhambi na hatimaye kupata hukumu.
   3.      Malezi mabaya: Biblia inasema katika MITHALI 22:6Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.” Kumbe mzazi au mlezi unanafasi kubwa ya kumpoteza mwanao. Mlee katika misingi sahihi ili asipotee.
   4.      Maneno yako yanaweza kuwakosesha wengine wakajikuta wamefanya mambo yasiyo stahili. Maneno ya uongo yanaleta hasira, chuki, kinyongo, fitina na hata visasi. Kwa mtu uliyemsababishia kinyongo au hasira maana yake umemkwaza, umemkosesha na kwa namna hiyo anahesabiwa katenda dhambi na kama mtu huyo atakufa katika dhambi hiyo damu yake itatakwa kwako.
   5.       Chakula: unaweza kuwakwaza watu kwa chakula. Mathalani wewe unapenda nyama fulani na mkeo au mmeo hapendi kabisa kuiona au kuigusa nyama hiyo jambo la kufanya ni kwamba, kwa kuwa wewe unaipenda sana nyama hiyo au chakula hicho nenda mahali wanapouza nunua, tumia kisha rejea nyumbani na usitumie mbele ya mmeo/mkeo asiyekula nyama/chakula hicho kwani kwa kufanya hivyo unaleta makwazo bila sababu ya msingi. Biblia imeweka wazi kabisa suala hili. Ukisoma katika WARUMI 14:14-23 inasema 14 Najua, tena nimehakikishwa sana katika Bwana Yesu, ya kuwa hakuna kitu kilicho najisi kwa asili yake, lakini kwake yeye akionaye kitu kuwa najisi, kwake huyo kitu kile ni najisi. 15 Na ndugu yako akiingia huzuni kwa sababu ya chakula, umeacha kwenda katika upendo. Kwa chakula chako usimharibu mtu yule ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.16 Basi, huo wema wenu usitajwe kwa ubaya.17 Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu.18 Kwa kuwa yeye amtumikiaye Kristo katika mambo hayo humpendeza Mungu, tena hukubaliwa na wanadamu.19 Basi kama ni hivyo, na mfuate mambo ya amani na mambo yafaayo kwa kujengana. 20 Kwa ajili ya chakula usiiharibu kazi ya Mungu. Kweli, vyote ni safi; bali ni vibaya kwa mtu alaye na kujikwaza. 21 Ni vyema kutokula nyama wala kunywa divai wala kutenda neno lo lote ambalo kwa hilo ndugu yako hukwazwa. 22 Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.23 Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi.”

Pia 1 WAKORINTHO 10:31-32 inafafanua zaidi 31 Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu. 32 Msiwakoseshe Wayahudi wala Wayunani wala kanisa la Mungu,”  Kumbe hatupaswi kuwakosesha wengine kwa chakula hata vinywaji wasivyovitumia.


LUKA 17:1 1 Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake!

NB: Pamoja na kuwako mambo yakoseshayo, ewe kaka ewe baba usikubali kuvutwa kwenye uasherati au uzinzi. Ewe dada ewe mama usikubali mazingira kukufanya umuache Mungu, iwe ni kazini boss wako anataka kufanya uasherati au uzizinzi na wewe ili upate kazi, cheo n.k…….  Usikubali jambo lolote 
likutenge na upendo wa Kristo. (WARUMI 8:35)
Ni ole kwako wewe uletaye makwazo/mambo ya kukosesha.

GROUP LA FACEBOOK: INJILI HALISI MINISTRY

Pakua App Ya Injili Halisi -Bofya Hapa Flower
HII NI INJILI HALISI MINISTRY, KWA MAWASILIANO +255 621 261 295

About INJILI HALISI MINISTRY

Zachary, most known as Zakacheka is the founder of the Injili Halisi Ministry. He is a member of Full Gospel Bible Fellowship Church.. He lives in Mwanza,Tanzania. 0621261295.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply