» » JE, YUDA ALIENDA MBINGUNI AU MOTONI??


Moja ya swali linaloulizwa na wakristo wengi ni, Je, Yuda alienda Mbinguni au Jehanum?
Biblia imeweka wazi kwamba Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu sasa yuko motoni. Yuda Iskariote hakuwa ameokoka ingawa alihuzunika kabla ya kwenda kujinyonga lakini hakutubu.

Mungu hakumuumba Yuda ili aje kumsaliti Yesu, lakini alijua kwamba atafanya hivyo. Kumbuka hata leo kuna baadhi ya watu wasio wakristo halisi wa leo hii  wanalitumia jina la Mungu ili kujipatia pesa na naamini hata Yuda pia alimtumia Yesu ili kujipatia pesa pekee wala hakuwa na mpango naye (Yohana 10:28).

Zifuatazo ni sababu zinazothibitisha kwamba Yuda hakwenda Mbinguni:-

1. Yuda alikuwa ni mwizi mwenye tamaa, alimsaliti Yesu kwa ajili ya pesa!
Yohana 12:4-6Basi Yuda Iskariote, mmojawapo wa wanafunzi wake, ambaye ndiye atakaye kumsaliti, akasema, Mbona marhamu hii haikuuzwa kwa dinari mia tatu, wakapewa maskini? Naye aliyasema hayo, si kwa kuwahurumia maskini; bali kwa kuwa ni mwivi, naye ndiye aliyeshika mfuko, akavichukua vilivyotiwa humo.


1 Wakorintho 6:9-10 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.”


Mathayo 26:14-16 “Wakati huo mmoja wa wale Thenashara, jina lake Yuda Iskariote, aliwaendea wakuu wa makuhani, akasema, Ni nini mtakachonipa, nami nitamsaliti kwenu? Wakampimia vipande thelathini vya fedha.Tokea wakati huo akawa akitafuta nafasi apate kumsaliti.


Luka 16:13 “Hakuna mtumishi awezaye kutumikia mabwana wawili…..Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.”

2. Yuda alikuwa ameokoka? Hapana, Shetani alimuingia. Mkristo halisi hawezi kuvamiwa na mapepo!

Yohana 13:27-30 “Na baada ya hilo tonge Shetani alimwingia. Basi Yesu akamwambia, Uyatendayo yatende upesi. Wala hakuna mtu katika wale walioketi chakulani aliyeijua sababu ya kumwambia hivyo. Kwa maana wengine walidhania, kwa kuwa Yuda huchukua mfuko, ya kwamba Yesu alimwambia kama, Nunua mnavyovihitaji kwa sikukuu; au kwamba awape maskini kitu. Basi huyo, akiisha kulipokea lile tonge, akatoka mara hiyo. Nako kulikuwa ni usiku.”


 1 Yohana 5:18 “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.”



3. Yesu alimuita Yuda kuwa amemchagua akiwa ni ‘Shetani’!
Yohana 6:70 “Yesu akawajibu, Je! Mimi sikuwachagua ninyi Thenashara, na mmoja wenu ni shetani?”


4.Yesu alitambua kuwapo kwa Yuda duniani ilikuwa ni hasara kawke Yuda mwenyewe
 Mathayo 26:20-24  “Basi kulipokuwa jioni aliketi chakulani pamoja na wale Thenashara.  Nao walipokuwa wakila, alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu atanisaliti.  Wakahuzunika sana, wakaanza kumwuliza mmoja mmoja, Ni mimi, Bwana? Akajibu akasema, Yeye aliyetia mkono wake pamoja nami katika kombe, ndiye atakayenisaliti. Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa.”

5. Yuda alikuwa ndiye mchafu kati ya wanafunzi wa Yesu. Hakuwa amesamehewa dhambi zake.
 Yohana 13:8-11 “Petro akamwambia, Wewe hutanitawadha miguu kamwe. Yesu akamwambia, Kama nisipokutawadha, huna shirika nami. Simoni Petro akamwambia, Bwana, si miguu yangu tu, hata na mikono yangu na kichwa changu pia. Yesu akamwambia, Yeye aliyekwisha kuoga hana haja ila ya kutawadha miguu, bali yu safi mwili wote; nanyi mmekuwa safi, lakini si nyote. Kwa maana alimjua yeye atakayemsaliti; ndiyo maana alisema, Si nyote mlio safi.”

6. Yuda hakumwamini wala hakumjua Yesu kuwa ni nani
Ingawa Yuda alihuzunika kwa kumsaliti Yesu, hakuamini kuwa Yesu alikuwa ni nani hasa.
Yohana 6:64-65  " Lakini kuna wengine miongoni mwenu wasioamini. Kwa maana Yesu alijua tangu mwanzo ni nani wasioamini, naye ni nani atakayemsaliti. Akasema, Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”

HITIMISHO: Kutokana na maandiko, tunahitimisha kwamba, Yuda hakuwa mwamini wa kweli katika Kristo (Yohana 6:64), kwa sababu hiyo aliingiwa na Shetani na hali hii inaonesha ni jinsi gani hali yake ya kiroho ilivyokuwa mbaya (Yohana 13:27),  pamoja na kujuta baada ya kumsaliti Yesu lakini hakutubu na Yesu alisema heri asingezaliwa mtu aakaye msaliti, maana yake kuzaliwa kwake hakukuwa na faida (Mathayo 26:24Marko 14:21).   Kwa hiyo, tunahitimisha kwa kusema Yuda alienda Jehanum.

GROUP LA FACEBOOK: INJILI HALISI MINISTRY







Pakua App Ya Injili Halisi -Bofya Hapa Flower
HII NI INJILI HALISI MINISTRY, KWA MAWASILIANO +255 621 261 295

About INJILI HALISI MINISTRY

Zachary, most known as Zakacheka is the founder of the Injili Halisi Ministry. He is a member of Full Gospel Bible Fellowship Church.. He lives in Mwanza,Tanzania. 0621261295.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply