» » UNABII WA MWEZI DESEMBA


 
Mwezi DESEMBA katika biblia zetu unasomwa kama mwezi wa Kenda/tisa ambao kwa Kiebrania unaitwa KISLEV(KISLEU) na wakati mwingine katika biblia zetu utakuta umeandikwa Kisleu.
KISLEV ni mwezi wa tatu wa Serikali na ni mwezi wa tisa wa mwaka wa Kiyahudi katika kalenda ya Kiebrania. KISLEU ni mwezi wa majira ya VULI ambao ni kati ya  mwezi Novemba na Desemba kwa kalenda ya Gregorian.

Tunaona katika NEHEMIA 1:1    “1 Habari za Nehemia, mwana wa Hakalia. Ikawa katika mwezi wa Kisleu, mwaka wa ishirini, nilipokuwapo Shushani ngomeni,”

Pia katika ZEKARIA 7:1 “1 Ikawa katika mwaka wa nne wa mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, siku ya nne ya mwezi wa kenda, yaani, Kisleu.”

Huu ni mwezi wa kubarikiwa na Mungu  kama tunavyoona katika HAGAI 2:18-19 “18 Tafakarini, nawaomba; tangu siku hii ya leo na siku zijazo; tangu siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kenda, naam, tangu siku hiyo ulipowekwa msingi wa hekalu la Bwana tafakarini haya. 19 Je! Mbegu ingali ghalani? Naam, huo mzabibu, wala mtini, wala mkomamanga, wala mzeituni, haikuzaa kitu; tangu siku hii ya leo nitawabariki.”

Huu ni mwezi wa ndoto kutimia na huu ni mwezi wa maono chanya.

Ni vyema tukafahamu ili Mungu awabariki watu wake kuna kuwa na mambo aliyoagiza. Mambo hayo tunayaona katika ZEKARIA 8:9 “9 Bwana wa majeshi asema hivi, Mikono yenu na iwe hodari, ninyi mnaosikia siku hizi maneno haya kwa vinywa vya manabii, waliokuwapo siku hiyo ulipowekwa msingi wa nyumba ya Bwana wa majeshi; yaani, hekalu hilo; ili lijengwe.”
Hapo tumeona mikono inakuwa hodari kwa wanaoisikia sauti ya Mungu yaani neno la Mungu kupitia vinywa vya watumishi wake. Hivyo basi mwezi huu ukijiweka vizuri na Mungu kwa kulisikia neno lake na kulitenda hakika ndoto zako ulizokuwa nazo kwa muda mrefu huu ndio mwezi wa kupokea kutoka kwa Bwana.

Pia katika NEHEMIA 1:1,9 inasema “1 Habari za Nehemia, mwana wa Hakalia. Ikawa katika mwezi wa Kisleu, mwaka wa ishirini, nilipokuwapo Shushani ngomeni, 9 bali mkinirudia mimi, na kuzishika amri zangu na kuzitenda, watu wako waliofukuzwa wajapokuwa katika pande za mwisho za mbingu, hata hivyo nitawakusanya kutoka huko, na kuwaleta mpaka mahali pale nilipopachagua ili kuliweka jina langu hapo.”

Huu ni mwezi hatari kwa kila atendaye mambo haya tunayoyaona katika ZEKARIA 7:8-12 8 Kisha neno la Bwana likamjia Zekaria, kusema, 9 Bwana wa majeshi amesema hivi, ya kwamba, Fanyeni hukumu za kweli, kila mtu na amwonee ndugu yake rehema na huruma; 10 tena msimdhulumu mjane, wala yatima, wala mgeni, wala maskini; wala mtu awaye yote miongoni mwenu asiwaze mabaya juu ya ndugu yake moyoni mwake. 11 Lakini hao walikataa kusikiliza, wakageuza bega lao, wakaziba masikio yao ili wasisikie. 12 Naam, walifanya mioyo yao kuwa kama jiwe gumu, wasije wakaisikia sheria na maneno ya Bwana wa majeshi, aliyoyapeleka kwa roho yake kwa mkono wa manabii wa kwanza; kwa sababu hiyo ghadhabu kuu ikatoka kwa Bwana wa majeshi.”.
Hapa tunaona ghadhabu iliyowapata watu waliokataa kusikia neno la Mungu.

Katika mwezi huu yeyote anayekataa kuisikia sauti ya Mungu atanyang’anywa mamlaka yake na kupewa mtu mwingine. Mali zake na vitu vyake vyote vitaharibiwa.

HAGAI 2:20-23 “20 Kisha neno la Bwana likamjia Hagai mara ya pili, siku ya ishirini na nne ya mwezi, kusema, 21 Sema na Zerubabeli, liwali wa Yuda, ukisema, Nitazitikisa mbingu na dunia; 22 nami nitakipindua kiti cha enzi cha falme, nami nitaziharibu nguvu za falme za mataifa; nami nitayapindua magari, na hao wapandao ndani yake; farasi na hao wawapandao wataanguka chini; kila mtu kwa upanga wa ndugu yake. 23 Katika siku ile, asema Bwana wa majeshi, nitakutwaa wewe, Ee Zerubabeli, mtumishi wangu, mwana wa Shealtieli, asema Bwana, nami nitakufanya kuwa kama pete yenye muhuri; kwa kuwa nimekuchagua, asema Bwana wa majeshi.”

Katika mwezi huu ni uamuzi wako kubarikiwa au kulaaniwa


Pakua App Ya Injili Halisi -Bofya Hapa Flower
HII NI INJILI HALISI MINISTRY, KWA MAWASILIANO +255 621 261 295

About INJILI HALISI MINISTRY

Zachary, most known as Zakacheka is the founder of the Injili Halisi Ministry. He is a member of Full Gospel Bible Fellowship Church.. He lives in Mwanza,Tanzania. 0621261295.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply