» »Unlabelled » DHAMBI YA KUWADHARAU WENGINE


Text Box: SOMO: AMDHARAUYE MWENZAKE 
AFANYA DHAMBI

 







Na Ev. Zachary John Bequeker (+255625966236)

Kumdharau mtu ni tabia ya kutomthamini, kutomheshimu na kumpuuza.
MITHALI 14:21 “Amdharauye mwenzake afanya dhambi; Bali amhurumiaye maskini ana heri.”
Katika andiko hili limejipambanua waziwazi kwamba dharau ni dhambi.    
         
Kwa nini dharau ni dhambi?
Dharau ni dhambi kwa sababu neno la Mungu limetuagiza tupendane katika Yohana 15:12 “Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi.”       Si rahisi kumpenda mtu usiyemheshimu. Kumbe palipo dharau hakuna upendo.
Kama mtu humpendi huwezi kuumia juu yake.Mungu kwa kuupenda ulimwengu wa dhambi akawa tayari kumtoa mwanae wa pekee Yesu Kristo, na si hivyo tu bali pia Yesu Kristo kwa upendo wake akawa tayari kujitoa ili afe kwa ajili ya dhambi zetu. Yesu alitutanguliza kwanza sisi akatuona kuwa ni wa thamani kwake hivyo hatupaswi tuangamie. Kumbe na sisi tukipendana, tutaheshimiana na kila mmoja atamtanguliza mwenzie. Tujifunze kuwaona wengine kuwa ni bora kuliko sisi.
WARUMI 12:10 Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu

Kuna watu tumekuwa tukijiona kuwa ni bora kuliko wengine kazini, kanisani, katika familia, ukoo au taifa pia. Kujiona kuwa ni bora kuliko wengine ni kujihesabia haki. Mungu humshusha mtu anayejiona kuwa ni bora kuliko wengine, tena huwashusha hata kuzimu(motoni) kwa sababu dharau ni dambi.

Neno linasema katika 1 Wathesalonike 5:14 kwamba “…. watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote.” Tunapaswa kuwatia moyo wale tunaoona ni dhaifu, duni wala hawawezi kuliko kuwasema na kuwadharau bure.

Tunapaswa kuchukuliana na walio dhaifu. Mfano ni kazini, kanisani au katika familia usifikiri wote mtakuwa na uwezo sawa katika utendaji, wewe utakuwa bora katika hiki lakini pia hata hao unao waona kuwa ni dhaifu watakuwa ni hodari katika jambo fulani ambalo wewe huliwezi; usiwadharau, watie moyo yaani watie nguvu kwa wanachokifanya na uwape mbinu mbadala ili wafanye vyema zaidi kuliko kuwasema tu. Kumbuka kila mmoja hutenda jambo kwa uwezo wake aliojaliwa(1 PETRO 4:11).
Hebu tuchukuliane na wale walio dhaifu wala tusitake wafanye kama tulivyo sisi. Ni vyema kutamani watu wengine wawe katika viwango ulivyonavyo vya utendaji au vya kiroho lakini kumbuka kwamba kila mmoja amejaliwa kwa namna yake. Ndio maana Paulo mtume wakati mmoja alitamani watu wasioe na kuolewa lakini hakulazimisha baada ya kutambua kuwa kuna wachache waliojaliwa wala si wote. Hivyo kumbe basi katika kazi, kanisa, familia au uongozi tusitegemee kuona wote tukiwa tunatenda kwa namna moja, huyu atakuwa hivi na yule vile.

Neno la Mungu linatuhimiza tuchukuliane wala tusidharauliane. Kuna watu wamekuwa wakiwadharau watumishi wa Mungu wa Mbinguni aliye hai na kujiona kuwa wao ni bora, wengine mmekuwa mkiona kuwa dhehebu lenu ndio bora kuliko mengine na kwa namna hiyo mmekuwa ni watu wa mipasho tu badala ya kumhubiri Kristo kama isemavyo 1 Wakorintho 1:23-24 mmekuwa ni watu wa kuyahubiri madhehebu yenu, mmekuwa ni watu wa kuhubiri mitazamo yenu wala si neno la Mungu. Ndugu zangu tusidharauliyane tukijua kwamba kwa maneno yetu tutahukumiwa (MATHAYO 12:37). Kumbuka yule mtumishi kipindi anapata maono ya kuanzisha huduma wewe hukuwepo na hata kama ulikuwepo huwezi fahamu vyema anayeujua ukweli ni mwanzilishi wa huduma wengine tutabaki kupiga kelele bure.

WAFILIPI 2:3-5 “Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu”
WAGALATIA 6:1-5 “1 Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.2 Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.3 Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake. 4 Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake. 5 Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.”

Siri ya kuinuliwa na Mungu ni kukubali kujishusha nakujitoa kwa ajili ya hao na kwa jinsi hii Mungu atapendezwa nasi (MATHAYO 22:25-28) .
Tujifunze namna ya kuwasaidia hao tunaowaona kuwa ni dhaifu ili wawe hodari na kwa jinsi hii tutang’aa (DANIELI 12:3).

Usimdharau ndugu yako, mfanyakazi menzako, kiongozi mwenzio wa dini, mshirika mwenzio kanisani, jirani yako au yeyote yule kumbuka hana apendaye awe dhaifu. Usidharau dhehebu fulani au watu wa dhehebu fulani. Ukiona wako kinyume na utaratibu  unapaswa kufanya mambo yafuatayo; moja waombee, pili sema nao wala hupaswi kujipiga kifua na kujidai, Mungu atakuhesabu kuwa wewe ni mpumbavu. Wewe unayejiona ni tajiri usiwadharau maskini na pia wafundishe watoto wako wawaheshimu watoto wa maskini na kuwaona nao ni binadamu kama wao.
LUKA 18:9-14 “9 Akawaambia mfano huu watu waliojikinai ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote… Yule Farisayo akasimama akiomba hivi moyoni mwake; Ee Mungu, nakushukuru kwa kuwa mimi si kama watu wengine, wanyang'anyi, wadhalimu, wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. 12 Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.13 Lakini yule mtoza ushuru alisimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua macho yake mbinguni, bali alijipiga-piga kifua akisema, Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.14 Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.”
INJILI HALISI MINISTRY (Online Ministry)
+255 625966236/ +255 758590489 / +255 67590489
Jifunze zaidi hapa =è zakachekainjili.blogspot.com

FB_IMG_1566146487568.jpg

Pakua App Ya Injili Halisi -Bofya Hapa Flower
HII NI INJILI HALISI MINISTRY, KWA MAWASILIANO +255 621 261 295

About INJILI HALISI MINISTRY

Zachary, most known as Zakacheka is the founder of the Injili Halisi Ministry. He is a member of Full Gospel Bible Fellowship Church.. He lives in Mwanza,Tanzania. 0621261295.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply